Saturday, September 5, 2020

MESSI KUSALIA BARCA NI NDOTO?

 


Mgombea wa wadhfa wa urais katika klabu ya Barcelona Victor Font anasema kwamba itakuwa hatua ya kushangaza lakini nzuri iwapo Lionel Messi atasalia na mabingwa hao wa Uhispania.

Messi mwenye umri wa miaka 33 wiki iliopita aliambia Barcelona kwamba anataka kukamilisha hudumu zake za miaka 20 katika klabu hiyo msimu huu.

Ripoti za hivi karibuni zimesema kwamba mchezaji huyo wa Argentina huenda akasalia katika klabu hiyo , lakini Font anasema kwamba uwezekano ni mchache.

''Atatushangaza kwasababu inaonekana tayari ameafikia uamuzi'', alisema Font.

Messi na Barcelona wapo katika mzozo kuhusu kifungu cha kandarasi yake na iwapo hana haki ya kuondoka katika klabu hiyo kama mchezaji huru.

Klabu zinazomuhitaji zinaitaka Barcelona kukubali dau lililo chini ya kifungu hicho cha kandarsi yake kinachotaka Barcelona ilipwe Yuro milioni 700 ilio kuondoka.

No comments: